Shirika la afya duniani WHO limetangaza kuwa maambukizi ya virusi vipya vya nimonia aina ya 2019-nCoV nchini China, hayajafikia kiwango cha tukio la dharura la afya ya umma linalofuatiliwa na dunia PHEIC.
Mkutano wa dharura wa WHO uliofanyika jana umetangaza baada ya majadiliano, kuwa ni mapema kwa sasa kuyatangaza maambukizi hayo kuwa ni tukio la dharura la afya ya umma linalofuatiliwa na dunia, sababu kuu ni kwamba idadi ya watu wanaoambukizwa virusi hivyo nje ya China ni wachache, na serikali ya China imetekelezwa hatua madhubuti za kinga na udhibiti.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |