Imesema imekuwa ikitoa mafunzo ya ukadiriaji kodi kwa wafanyakazi wake ili kumwezesha mfanyabiashara alipe kodi ya biashara yake kwa uhalali.
Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Msafiri Mbibo, aliyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati mkutano kati ya wafanyabiashara wakubwa na TRA uliolenga kuboresha uhusiano kati yao.
Alisema TRA pia imeweza kuboresha uhusiano na wafanyabiashara wakubwa kwa kuwa nao karibu wakati wote.
Aidha, alisema vigezo vinavyotumika kuwatenganisha wafanyabiashara wadogo, wakati na wakubwa ni mapato ghafi yanayozalishwa na mfanyabiashara, viwango vya ajira vinavyotolewa na mfanyabiashara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |