• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Zahera asema sababu nyingine ya kuachana na Yanga ni ujio wa kocha Charles Boniface Mkwasa

    (GMT+08:00) 2020-01-24 19:33:59

    Kocha wa zamani ya klabu ya Yanga, Mwinyi Zahera ameeleza sababu nyingine iliyopelekea kuachana na timu hiyo kuwa ni ujio wa kocha Charles Boniface Mkwasa. Zahera amesema alikubali kuachana na Yanga baada ya kuambiwa kuwa awe tayari nafasi ya kocha wake msaidizi, Noel Mwandila ichukuliwe na Charles Mkwasa. Aidha Zahera ameishauri Yanga kuwa isimuweke Mkwasa katika benchi la ufundi la timu na badala yake imuajiri kama Mkurugenzi wa Ufundi kutokana na heshima na utaalamu alio nao na kumuacha kocha mkuu afanye kazi na kocha msaidizi anayemtaka.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako