• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Benki ya Kilimo yatakiwa kufika vijijini

    (GMT+08:00) 2020-01-30 15:55:52

    Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini Tanzania (TADB) imtakiwa kuhakikisha inafikisha huduma zake maeneo ya vijijini ili wakulima waweze kunufaika nayo pamoja na kukuza uchumi wa viwanda kupitia mazao ya kimkakati.

    Akizungumza na radio China kimataifa, Mwenyekiti wa Chama cha Wenye Viwanda, Biashara na Kilimo (TCCIA) wilayani Moshi Bw Louis Mbuya amesema benki hiyo ikisogeza huduma zake vijijini wakulima wengi wataweza kulima kwa tija na kuwa na uhakika wa mavuno ambayo ni malighafi tosha kwa viwanda vya ndani na nje ya nchi.

    Alisema miaka ya nyuma wakulima wa kahawa walikuwa wakinufaika na Chama Kikuu cha Ushirika (KNCU) kwa kupewa pembejeo, lakini siku hizi hawatoi hivyo benki ya wakulima ndio itabaki kuwa mkombozi.

    Aliongeza kuwa kama TADB itajisogeza kwa wakulima, viwanda vingi vitakavyoanzishwa vitakuwa na uhakika wa kupata malighafi ndani ya nchi kutokana na wakulima wengi kulima kisasa hivyo kuwa na uhakika wa mazao.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako