Mtanzania Eliuter Mpepo anayecheza kwa mkopo soka ya kulipwa katika club ya CD Costa Do Sol ya nchini Msumbiji akitokea club ya A.D Sanjoanense ya Serea B nchini Ureno, amefanikiwa kutwaa Ngao ya Jamii na timu yake nchini Msumbiji. Mchezo wa Ngao ya Hisani (Community Shield) kati ya CD Costa dhidi ya UD Songo ulichezwa na dakika 90 zikamalizika kwa timu hizo kutoka sare ya kufungana 1-1. Mikwaju ya penati ndio ikaamua mshindi na CD Costa Do Sol kuibuka wababe wa Ngao ya Hisani kwa ushindi wa penati 7-6, mtanzania Eliuter Mpepo akipiga penati ya mwisho ya ushindi kwa timu yake ya CD Costa Do Sol.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |