Waziri mkuu wa Tanzania Bw. Kassim Majaliwa ameliambia bunge kuwa tume ya uchaguzi ya hivi sasa ni huru sana, huku akipinga wito lililotolewa na vyama vya upinzani kuhusu kuunda tume huru ya uchaguzi wanayosema itakuwa huru. Bw. Majaliwa amesema hayo akijibu hoja ya kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni Bw. Freeman Mbowe, huku akiongeza kuwa tume ya uchaguzi ya taifa ya nchi hiyo ni huru kama ilivyoelekezwa na katiba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |