Katika msaada mwingine wa sera ya kiufundi, IMF pia imeishauri serikali kuweka kipaumbele utekelezaji wa mkakati mpya wa uhamasishaji mapato ya ndani, inayolenga kuongezeka kwa uwiano wa ushuru hadi Mapato ya Taifa GDP kwa asilimia 0.5 kwa mwaka.
Ushauri huo wa IMF unakuja wakati serikali inapambana kupata mapato ya ndani kufadhili bajeti ya 2019/20, ambayo tayari imeona serikali ikikabiliwa na upungufu wa ukusanyaji wa mapato wa zaidi ya Sh bilioni 600 kwa sababu ya kuchelewesha utekelezaji wa hatua za ushuru wa ndani .
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |