Mwanariadha Mkenya, David Barmasai Tumo ameibuka mshindi wa mbio za Lagos City Marathon 2020 zilizotimua vumbi Jumamosi, Februari 8. Mbio hizo za kilomita 42 ambazo zilinoa nanga katika uwanja wa kitaifa eneo la Surulere, jimbo la Lagos, zilimshuhudia David Barmasai Tumo akikata utepe Eko Atlantic katika muda wa saa 2:10:23. Barmasai, ambaye ana miaka 31 aliweka kibindoni KSh 5 milioni baada ya kushinda mbio hizo za kilomita 42.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |