China ilikuwa imeweka sheria kali kwa raia wake ya kutotangamana au hata kutoka nje kama njia moja ya kukabili virusi hivi. Biashara nyingi zilifungwa na hivyo kuathirika pakubwa tangu kugunduliwa kwa virusi hivi vya Korona.
Shirika la Afya Duniani WHO limetuma wataalam wa afya kwenda Beijing kuchunguza hali halisi ya virusi hivi.
Kumekuwa na hofu kwamba kuendelea kufungwa kwa kampuni na viwanda nchini China, ambayo ni ya pili ulimwenguni kwa ukubwa kiuchumi, kungeathiri uchumi wa mataifa mengi duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |