Beki wa kati wa Kagera Sugar, Erick Kyaruzi amesema licha ya kufanya vizuri msimu huu wa Ligi Kuu, lakini ndoto yake bado haijatimia ya kuichezea timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, jambo ambalo linamuumiza. Mchezaji huo amekuwa katika kiwango kizuri katika msimu huu ambapo amesaidia timu yake kuwa katika nafasi ya nne wakiwa na point 34. Kyaruzi amesema ataendelea kujituma ili kutimiza lengo hilo kwani amecheza Ligi Kuu kwa takriban miaka mitano, lakini hajapata nafasi ya kucheza Taifa Stars.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |