Beckham amaliza mchezo, Neymar kutua Inter Miami
(GMT+08:00) 2020-02-12 18:25:00
David Beckham amekamilisha bonge la dili katika klabu yake ya Inter Milan baada ya kufanikiwa kunasa saini ya mshambuliaji wa PSG, Neymar, ambaye amekubali kutua kwenye klabu hiyo ya Ligi Kuu Marekani miaka 10 ijayo. Wakati Barcelona na Real Madrid zikipambania saini yake, Mbrazil huyo amefanya makubaliano na Beckham ambaye ni mmiliki wa Inter Milan kuwa atajiunga na timu hiyo kabla hajastaafu soka.