• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yatoa mwito wa kuwalinda watoto kwa kupitia utatuzi wa migogoro

    (GMT+08:00) 2020-02-13 09:46:10

    Mwakilishi wa kudumu wa China kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Zhang Jun ametoa mwito wa kuwalinda watoto kwenye migogoro ya kijeshi kupitia utatuzi wa migogoro.

    Balozi Zhang amesema njia ya kimsingi ya kuwalinda watoto kutokana na madhara ya migogoro ya kijeshi ni kusitisha na kutatua migogoro hiyo.

    Kwenye mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu watoto na migogoro ya kijeshi wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa Dhidi ya Matumizi ya Askari Watoto, Balozi Zhang amesema Migongano inapaswa kutatuliwa kwa njia ya mazungumzo ya usawa, na matumizi au matishio ya nguvu ya kijeshi lazima yaachwe, na jumuiya ya kimataifa inatakiwa kuzingatia kuzuia migogoro na kuhimiza mchakato wa amani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako