Shirika la Afya Duniani WHO limetangaza kuwa maambukizi ya Ebola nchini DRC yanayoanza mwezi Agosti mwaka 2018 bado ni dharura ya afya ya umma inayotia wasiwasi jumuiya ya kimataifa PHEIC.
Mkurugenzi mkuu wa WHO Bw. Tedros Ghebreyesus amesema kwenye taaifa kuwa uamuzi huo ni maoni ya pamoja ya kamati ya dharura ya WHO.
Wasiwasi mkuu wa WHO ni kwamba kuondoa hali ya dharura kwa ugonjwa huo kwa sasa huenda kukaleta athari mbaya kwa juhudi za kukabiliana na Ebola kutokana na kupunguza ufuatiliaji, hususan milipuko ya magonjwa mengine inayoendelea nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |