Wanasoka wa Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambao hawajapokea mishahara kwa muda mrefu kutoka kwa waajiri wao huenda wakapata afueni hivi karibuni. Hii ni baada ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) na Muungano wa Wanasoka Duniani (FIFPRO) kuanzisha mfuko wa fedha wa FIFA FFP utakaoshughulikia masilahi ya wachezaji ambao hawajalipwa au ambao dalili zinaashiria kwamba hawatalipwa na klabu zao duniani. FIFA imetenga kiasi cha Sh bilioni 1.6 ambazo zitawekwa katika Mfuko huo hadi mwisho wa mwaka 2022 ambapo mgao wa fedha hizi utafanyika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |