Rais Xi Jinping wa China leo amezungumza na waziri mkuu wa Malaysia Mahathir Bin Mohamad kwa njia ya simu.
Katika mazungumzo yao, rais Xi amesema, wakati Wachina wanapopambana na maambukizi ya COVID-19, waziri mkuu wa Malaysia amependekeza mazungumzo hayo, ikimaanisha urafiki na uungaji mkono wa Malaysia kwa China.
Rais Xi amesema ingawa maambukizi hayo yameathiri mawasiliano ya watu kati ya nchi hizo kwa muda, lakini hayataathiri urafiki mkubwa kati yao. Wakati China na Malaysia zinaposhirikiana kukabiliana na maambukizi, zinapaswa kukuza zaidi uhusiano kati yao, haswa ushirikiano wa kujenga kwa pamoja "Ukanda Mmoja, Njia Moja", ili kuwanufaisha wananchi wa nchi hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |