• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania yasaini mkopo wa dola za kimarekani bilioni 1.46 kwa ajili ya ujenzi wa reli ya SGR

    (GMT+08:00) 2020-02-14 19:01:08
    Tanzania imesaini makubaliano ya mkopo wa dola za kimarekani bilioni 1.46 na Beki ya Standard Chartered tawi la Tanzania ili kuwezesha ujenzi wa kilomita 550 za njia ya reli ya SGR kati ya mji wa kibiashara wa Dar es Salaam na katikati ya nchi hiyo.

    Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Fedha na Mipango ya Tanzania na Benki Standard Chartered tawi la Tanzania imesema, fedha hizo zitatumika kujenga sehemu yenye urefu wa kilomita 550 za reli kati ya Dar es Salaam na Makutupora, katikati ya Tanzania.

    Msemaji wa wizara ya Fedha Bw. Ben Mwaipaja amesema, mkopo huo uliosainiwa jana utalipwa katika kipindi cha miaka 20, lakini hakutoa taarifa zaidi juu ya kiwango cha riba.

    Utakapokamilika, mtandao huo wa reli utaiunganisha Tanzania na Burundi, Rwanda, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako