• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Marekani yaongeza muda wa siku 45 wa kufanya biashara na kampuni ya Huawei nchini humo

    (GMT+08:00) 2020-02-14 19:21:41

    Wizara ya biashara ya Marekani jana imesema, serikali ya nchi hiyo inairuhusu kampuni ya Huawei ya China inunue bidhaa na huduma za Marekani kwa siku 45 nyingine, ili kupunguza athari mbaya kwa makampuni na wateja wa Marekani.

    Taarifa iliyotolewa na Wizara hiyo imesema, hatua hiyo itayawezesha makapuni ya TEHAMA ya Marekani hasa kwa yale vijijini kuwa na uwezo wa kuendelea kuendesha mtandao uliopo wa internet kwa usalama.

    Hii ni mara ya nne kwa serikali ya Trump kuongeza muda wa kuruhusu makampuni yake kufanya biashara na Huawei ya China tangu Marekani itoe amri ya kupiga marufuku dhidi ya Huawei mwezi Mei mwaka jana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako