• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Taakwimu za mifugo bado hazitoshi Tanzania

    (GMT+08:00) 2020-02-14 19:40:01
    Ukosefu wa takwimu sahihi za mifugo kwenye vijiji kumetajwa kuwa moja ya sababu za Serikali za Vijiji kushindwa kutenga maeneo ya malisho yanayokidhi mahitaji ya wafugaji katika maeneo mbalimbali nchini, hivyo kusababisha migogoro ya wafugaji na wakulima kuendelea.

    Hayo yalisemwa na wadau wa mifugo mkoani Mbeya wakati wa mkutano wenye lengo la kujadili matatizo yanayoikabili sekta hiyo pamoja na njia za kuzitatua ili kuiendeleza kwa maslahi ya taifa.

    Mkutano huo uliwakutanisha maofisa mifugo wa kata zote za Jiji la Mbeya, Watendaji wa Halmashauri na Maofisa kutoka katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

    Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Hassan Mkwawa, alisema takwimu za mifugo ni muhimu wakati wa kupanga matumizi bora ya ardhi katika eneo lolote nchini.

    Alisema maeneo mengi kwenye vijiji yanatengwa kwa ajili ya mifugo, lakini baada ya muda yanaonekana ni madogo kutokana na kutengwa bila kuwa na takwimu sahihi ya mifugo ya maeneo husika.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako