Hayo yalisemwa na wadau wa mifugo mkoani Mbeya wakati wa mkutano wenye lengo la kujadili matatizo yanayoikabili sekta hiyo pamoja na njia za kuzitatua ili kuiendeleza kwa maslahi ya taifa.
Mkutano huo uliwakutanisha maofisa mifugo wa kata zote za Jiji la Mbeya, Watendaji wa Halmashauri na Maofisa kutoka katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Hassan Mkwawa, alisema takwimu za mifugo ni muhimu wakati wa kupanga matumizi bora ya ardhi katika eneo lolote nchini.
Alisema maeneo mengi kwenye vijiji yanatengwa kwa ajili ya mifugo, lakini baada ya muda yanaonekana ni madogo kutokana na kutengwa bila kuwa na takwimu sahihi ya mifugo ya maeneo husika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |