Mkuu wa Tume ya uchaguzi ya Afghanistan Hawa Alam Nuristani ametangaza kuwa rais wa sasa Mohammad Ashraf Ghani amepata asilimia 50.64 ya kura kwenye uchaguzi mkuu, na kuwa rais wa nchi hiyo kwa muhula wa pili. Mpinzani wa Bw. Ghani ambaye ni mtendaji mkuu wa serikali ya Umoja wa Kitaifa Abdullah Abdullah amepata nafasi ya pili kwa kupata asilimia 39.52 ya kura.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |