Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imeunda Kamati ya Maendeleo ya Miradi ili kusimamia utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa vituo vya michezo vya Kigamboni, jijini Dar es Salaam na Tanga. Kabla ya kuunda Kamati hiyo, Kamati ya Utendaji ilipokea taarifa ya maandalizi ya utekelezaji wa miradi hiyo kwenye kikao chake kilichofanyika jumanne jijini Dar es Salaam. Wajumbe wa Kamati hiyo ni QS Lucy Mzengi (Mwenyekiti), Mhandisi Hersi Said, Mhandisi Hamad Ramadhan, na Mhandisi Charles Adrian.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |