Shirika la ndege la Iraq limesimamisha safari za ndege kwenda na kurudi kutoka Iran ikiwa ni hatua ya kuzuia maambukizi ya virusi vya COVID-19 baada ya kutokea nchini Iran. Uamuzi huo umetolewa na wizara ya uchukuzi baada ya wizara ya afya ya Iran kutoa mapendekezo ya kuchukua hatua za lazima za kuzuia maambukizi ya virusi hivyo nchini Iraq. Mapema ya siku hiyo, mamlaka ya Iraq imeamua kuwazuia wairan kuingia Iraq na wairaq kwenda Iran.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |