Japan imeahidi kuandaa mashindano ya Olimpiki ya Tokyo na mashindano ya Walemavu wakati wa msimu wa joto mwaka huu kama ilivyopangwa, licha ya hali ya maambukizi ya virusi vya korona kuwa mbaya zaidi. Katibu mkuu wa Baraza la Mawaziri nchini Japan Yoshihide Suga amesema, watafuatilia kwa karibu kwa pamoja na IOC, kamati ya maandalizi na serikali ya Tokyo, na kuendelea na maandalizi ili kuhakikisha wanariadha na watazamaji wanaweza kuwa salama wakati wa mashindano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |