Gazeti la Daily Mail limeripoti kuwa, huenda michezo ya Olimpiki ya Tokyo ikaahirishwa hadi mwishoni mwa mwaka huu, ikiwa ni katika jitihada za kuzuia kuenea kwa virusi vya korona. Waziri wa Olimpiki nchini Japan Seiko Hashimoto ameliambia bunge la nchi hiyo kuwa, makubaliano ya Japan na Shirikisho la Kimataifa la Olimpiki (IOC) linawaruhusu kuchelewesha kuanza kwa michezo hiyo. Amesema mkataba unataka mashindano hayo yafanyike ndani yam waka 2020, na kipendele hicho kinaweza kuchukuliwa kama kibali cha kuyaahirisha mashindano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |