Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litaitisha mkutano unaohusu amani na usalama wa Afrika wiki ijayo, huku likilenga zaidi mjadala kuhusu kupambana na ugaidi na misimamo mikali.
Balozi wa China katika Umoja wa Mataifa Bw. Zhang Jun ambaye pia ni mwenyekiti wa zamu wa mwezi Machi wa Baraza hilo amesema, bara la Afrika lina uwezo mkubwa wa maendeleo, lakini pia linakabiliana na changamoto nyingi, ikiwemo matishio ya ugaidi na misimamo mikali.
Bw. Zhang pia amesema, Baraza hilo linatarajia kupata utatuzi halisi kuhusu matatizo yaliyopo na kuifanyia jumuiya ya kimataifa kuyapa mashirika ya kikanda barani Afrika nafasi kubwa zaidi katika kukabliana na matishio hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |