Timu ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa wavu wa ufukweni ya wanaume imeingia kambini jijini Dar es Salaam kujiandaa na michuano ya Afrika hatua ya pili kufuzu michuano ya Olimpiki Tokyo 2020. Kocha wa timu hiyo, Alfred Selengia amesema timu yake inajiandaa na mashindano hayo ya Kundi B yenye timu za Ghana, Afrika Kusini, Sudan, Niger na wenyeji Tanzania. Mashindano hayo yanatazamiwa kuanza Machi 27 kwenye ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |