Waziri mkuu nchini Italia Giuseppe Conte amesaini pendekezo la kamati ya Olimpiki nchini Italia la kutaka michezo yote Italia ikiwemo Serie A kusimama kwa muda kutokana na mlipuko wa virusi vya korona. Kwa sasa Italia imeripotiwa kuwa Ligi Kuu ya Italia Serie A ni waathirika pia wa maambukizi hayo, Serie A imesimamishwa hadi April 3 2020. Conte amesema eneo lote la Italia linalindwa na kufungwa. Ligi zote zitasimama na Rais wa mikoa yote Italia amekubaliana na maamuzi haya, aidha amewapa pole mashabiki wote wa Serie A pia na kusema inawalazimu waisimamishe.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |