Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania ya mchezo wa Cricket, Steve Tikolo amesema kuwa kikosi chake kimekamilika kwa asilimia kubwa kupambana katika mashindano ya T20 yanayotarajiwa kufanyika mwezi ujao nchini Afrika Kusini. Kocha huyo ambaye ni raia wa Kenya amesema licha ya kubaini mapungufu kadhaa, amefurahishwa na kiwango kizuri kilichooneshwa na wachezaji wake. Tikolo amesema, tatizo alilobaini ni kushindwa kudaka mipira, kitu ambacho si kizuri katika mchezo huo, na hasa mashindano wanayokwenda kushiriki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |