Serikali ya Sudan imesema watuhumiwa waliohusika na jaribio la kumuua waziri mkuu wa nchi hiyo Bw. Abdalla Hamdok wamekamatwa.
Waziri wa Habari wa Sudan ambaye pia ni msemaji wa serikali Bw. Faisal Mohamed Saleh, amesema watuhumiwa kadhaa wakiwa ni pamoja na wageni wamekamatwa. Akiongeza kuwa timu ya usalama ya Marekani jana ilifika Khartoum na kushirikiana na wapelelezi wa Sudan kufanya uchunguzi. Pia amedokeza kuwa mipango mipya imetekelezwa katika kulinda usalama wa nchi hiyo, na polisi na idara ya upelelezi zimechukua hatua kuhakikisha usalama wa waziri mkuu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |