Wakati dunia ikiwa katika juhudi za kupambana na virusi hatari vya Corona, Tokyo yaendelea na mandalizi ya mashindano ya Olimpiki, licha ya WHO kutangaza rasmi kuwa virusi vya Corona ni janga la kimataifa. Jana, Japan ilisema itaendelea na maandalizi yake ya michezo ya olimpiki na ile ya michezo ya Olimpiki kwa walemavu kama ilivyopangwa hapo awali hata baada ya WHO kutangaza rasmi kuwa virusi vya corona ni janga la kimataifa. Wajumbe wa kamati ya mandalizi ya Tokyo pia wamesema kuwa mashindano ya Olimpiki yatafanyika kama ilivyopangwa. Takribani wanariadha 11,000 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |