Muasisi wa soka la wanawake nchini Tanzania Alhaj Dk Maneno Tamba amewataka wadau wa soka kumuonyesha thamani na heshima yake kabla hajatangulia mbele za haki. Dk Tamba amesema kutokana na umuhimu na mchango wake katika hilo, ni vyema akapewa heshima hiyo sasa. Amesema hata anapokwenda uwanjani anajilipia kiingilio mwenyewe n ahata akifika getini, hubughudhiwa wakati ana mchango mkubwa katika soka la wanawake nchini Tanzania.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |