Benki kuu ya Marekani jana ilipunguza kiwango cha riba kwa asilimia 1 na kufikia karibu na sifuri, na kuongeza dhamana zake kwa dola bilioni 700 za kimarekani, kutokana na mlipuko wa virusi vya korona. Benki hiyo imesema mlipuko wa virusi vya korona umeathiri jamii na shughuli za kiuchumi katika nchi nyingi ikiwemo Marekani, na kwamba hali ya kifedha duniani pia imeathiriwa vibaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |