Kocha Mkuu wa Azam FC, Aristica Cioaba amesema kutokuwa makini kwa washambuliaji wake ni sababu kubwa ya kushindwa kupata idadi kubwa ya magoli katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu. Amesema wachezaji wake wanashindwa kutumia nafasi wanazopata jambo linalowapa ugumu kuondoka na pointi tatu. Idadi kubwa ya magoli ambayo timu hiyo imepata ni pale iliposhinda 5 – 0 dhidi ya Alliance FC.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |