• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Nusu ya wagonjwa wa COVID-19 watoka hospitali ya Leishenshan ya Wuhan baada ya kupona

    (GMT+08:00) 2020-03-18 09:26:35

    Naibu mkurugenzi wa hospitali ya Leishenshan ya Wuhan Bw. Yuan Yufeng jana kwenye mkutano na waandishi wa habari amesema, karibu nusu ya wagonjwa wa COVID-19 waliopewa matibabu kwenye hospitali hiyo wameruhusiwa kutoka baada ya kupona.

    Bw. Yuan amesema, hadi kufikia Jumatatu, hospitali ya Leishenshan ilikuwa imepokea wagonjwa 1,961 wa COVID-19 na wagonjwa 970 kati yao wametoka. Bw. Yuan ameongeza kuwa, hospitali hiyo ina wafanyakazi wa matibabu 3,202 wa timu 16 za matibabu kutoka mikoa tisa, pamoja na wahudumu 660.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako