Naibu mkurugenzi wa hospitali ya Leishenshan ya Wuhan Bw. Yuan Yufeng jana kwenye mkutano na waandishi wa habari amesema, karibu nusu ya wagonjwa wa COVID-19 waliopewa matibabu kwenye hospitali hiyo wameruhusiwa kutoka baada ya kupona.
Bw. Yuan amesema, hadi kufikia Jumatatu, hospitali ya Leishenshan ilikuwa imepokea wagonjwa 1,961 wa COVID-19 na wagonjwa 970 kati yao wametoka. Bw. Yuan ameongeza kuwa, hospitali hiyo ina wafanyakazi wa matibabu 3,202 wa timu 16 za matibabu kutoka mikoa tisa, pamoja na wahudumu 660.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |