Uganda imezindua mradi wa miaka miwili unaolenga kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wakimbizi ili kuboresha maisha yao. Mkuu wa huduma za kifedha wa shirika moja lisilo la kiserikali la Uganda Bibi Juliet Tumuzoire, amesema hadi kufikia mwishoni mwa miaka hiyo miwili, wakimbizi wapatao laki 2 watapewa huduma za kifedha. Pia amesema mradi huo utahusisha kambi 5 za wakimbizi kati ya 28 nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |