Ili kupunguza maambukizi kupitia pesa taslimu,kampuni ya simu ya MTN ,nchini humo,imeanza hatua ambayo itapunguza ukamataji wa pesa taslimu na watu kufanya miamala na malipo kwa njia ya simu.
Kulingana na barua iliyoandikwa jana na Afisa Mkuu Mtendaji wa MTN,Bw William Vanhelleputte,kwenda kwa Idara ya Kitaifa ya Mifumo ya Malipo ya Benki Kuu ya Uganda ,majadiliano na Benki Kuu pamoja na benki zingine yalifanyika,na kusababisha ukuzaji na matumizi ya pesa kwa njia ya simu kuliko kukamata pesa taslimu kama njia moja ya kujikinga na maambukizi ya COVID-19.
Mojawapo ya mapendekeo yaliyoandikwa katika barua hiyo ni pamoja na kutokuwa na ada yoyote kwa miamala isiyozidi Sh30,000.
Katika hotuba yake wakati akihutubia Taifa siku ya jumatano,Rais Yoweri Museveni alisema Wizara ya Afya itatoa taratibu zinazofaa kuhusu miamala ya pesa,ikiwa ni pamoja na matumizi ya pesa kwa njia ya simu,kufanya manunuzi mitandaoni,miongoni mwa mengine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |