Waziri mkuu wa Canada Bw. Justin Trudeau amesema, mpaka kati ya nchi hiyo na Marekani huenda utafungwa kwa safari zisizo za lazima kuanzia leo usiku, ili kuzuia kuenea kwa COVID-19. Bw. Trudeau amesema hayo mjini Ottawa ambako amejiweka karantini baada ya mkewe kuthibitika kuambukizwa virusi hivyo wiki iliyopita. Bw. Trudeau pia amesema, wanazungumza na Marekani juu ya mambo ya mwisho.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |