• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kusitishwa kwa uvuvi haramu kwanufaisha wavuvi 

    (GMT+08:00) 2020-03-20 19:21:26
    Doria inayofanywa katika ukanda maeneo ya Hifadhi ya Kisiwa cha Tumbatu, Mkoa wa Kaskazini Unguja zinasemekana kusaidia kudhibiti uvuvi haramu na kuleta matumaini makubwa kwa wavuvi kupata mapato zaidi.

    Mkuu wa Doria kutoka Idara ya Maendeleo ya Uvuvi, Haji Shomari amesema doria hizo zimerudisha matumaini ya wavuvi kupata kipato kikubwa kufuatia kuwapo kwa hazina ya samaki baada ya eneo la ukanda huo kuingizwa katika orodha mpya ya hifadhi mwaka jana.

    Baadhi ya wavuvi wa ukanda wa ghuba ya hifadhi hiyo, walieleza kufurahishwa na doria hizo ambazo lengo lake ni kuzuia uvuvi haramu na kulinda rasilimali za baharini.

    Mradi huo uliopewa jina wa Swiofish unatekelezwa chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia ukiwa na lengo la kulinda rasilimali za baharini na kuwawezesha wavuvi wadogo kupiga hatua kimaendeleo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako