• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uchumi wa Marekani watarajiwa kushuka kwa asilimia 12 katika robo ya pili mwaka huu

     

    (GMT+08:00) 2020-03-20 19:24:29
    Mchumi wa shirika la Merrill Lync la Marekani Bi. Michelle Meyer jana alikadiria kuwa uchumi wa Marekani katika robo ya pili ya mwaka huu utashuka kwa asilimia 12, na idadi ya watu watakaokosa ajira itafikia milioni 3.5.

    Shirika la kimataifa la kutathmini dhamana la Moody nalo limesema, mpango wenye thamani ya dola za kimarekani trilioni 1 utakatolewa na serikali ya Marekani utaongeza shinikizo la madeni la nchi hiyo.

    Habari nyingine zinasema, benki kuu ya Marekani ilipanga kununua madeni ya taifa ya dola za kimarekani bilioni75 jana na leo kwa ajili ya kukabiliana na athari ya uchumi inayosababishwa na maambukizi ya virusi vipya vya Corona.

    Wizara ya nishati ya Marekani ilitangaza kununua mapipa milioni 30 ya mafuta ghafi yatakayotumika kwa mfuko wa mafuta ya kimkakati ya Marekani ambayo ni pungufu ya mapipa milioni 77 yaliyotangazwa awali.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako