Hatua hiyo imejiri siku moja tu baada ya Rais wa Uganda Yoweri Museveni kuamrisha kufungwa kwa mipaka yake, saa chache tu baada ya nchi hiyo kutangaza kisa chake cha kwanza cha Covid-19.
Akitoa taarifa jana kutoka Busia OSBP, Kamishna wa Kaunti Joseph Kanyiri, alisema kufungwa kwa vituo hivyo ni kwa maslahi ya raia wa mataifa hayo mawili.
Hii ni katika juhudi zinazolenga kuimarisha mikakati ya serikali ya kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona.
Hatua hiyo imejiri siku moja tu baada ya Rais wa Uganda Yoweri Museveni kuamrisha kufungwa kwa mipaka yake, saa chache tu baada ya nchi hiyo kutangaza kisa chake cha kwanza cha Covid-19. Kwa sasa, kupitia majadiliano na kamati za usimamizi wa mipaka katika vituo vya Busia na Malaba, trela zinazosafirisha mizigo katika pande husika zitaruhusiwa kuingia lakini zikiwa na wahudumu wawili pekee.
Hatua hii imewaathiri maelfu ya wafanyibiashara mpakani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |