Tume ya uchaguzi ya Malawi MEC imetangaza kuwa uchaguzi mpya wa rais wa Malawi utafanyika Julai 2 kufuatia uamuzi uliotolewa Februari 3 na Mahakama, kwamba uchaguzi unatakiwa kufanyika ndani ya siku 150. Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji Jane Ansah ametangaza uamuzi huo huko Blantyre, na kusema uteuzi wa wagombea wa urais unatarajiwa kufanyika Aprili 23 na 24.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |