Uongozi wa timu ya soka ya Polisi Tanzania umesema, kikosi chake kitarejea kambini Machi 30 ili kujiweka sawa kwa ajili ya kumalizia msimu wa 2019/20 wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Kocha Mkuu wa timu hiyo Hamsini Malale amesema, wameamua kuanza kambi mapema ili kuwaweka sawa wachezaji wake, huku wakisubiri tarehe mpya ya kuendelea kwa Ligi hiyo. Amesema maambukizi ya virusi vya Corona yamemwaribia mipango yake katika kukijenga kikosi hicho kuelekea mechi za hatua ya lala salama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |