China imefanikiwa kutuma seti ya satelaiti mpya za kuona mbali kwenye mzunguko wa dunia kutokea Kituo cha Kurusha Satellite cha Xichang, kusini mwa mkoa wa Sichuan nchini China.
Satelaiti hizo za familia ya Yaogan-30, zimerushwa leo saa tano na dakika 43 kwa saa za China, kwa kutumia roketi ya Long March-2C, na zitashughulikia ugunduzi wa mazingira ya kielektroniki na majaribio ya teknolojia zinazohusika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |