Mkoa unaojiendesha wa kabila la Wauyghur wa Xinjiang nchini China umetoa msaada wa mask 380,000 kwa nchi za Korea Kusini, Malaysia, Iran, Iraq, Lebanon, Tunisia na Algeria kuzisaidia kupambana na mlipuko wa virusi vya Corona.
Serikali ya mkoa wa Xinjiang imehimiza makampuni husika kuongeza utengenezaji wa mask. Aidha, forodha na posta ya China zimeshirikiana kuhakikisha malighafi zinazotumika katika kutengeneza mask zinafikishwa kwa wakati.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |