Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya mkutano kwa njia ya video kuhusu tume ya Umoja wa Mataifa nchini DRC na hali ya nchi hiyo. Mkutano usio rasmi umekuwa shughuli ya kwanza ya baraza hilo tangu Machi 13 na kufuata hatua zilizotangazwa na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres za kudhibiti maambukizi ya COVID-19 katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, ikiwa pamoja na kufunga baadhi ya ofisi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |