Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amemteua Bw. Guang Cong kutoka China kuwa naibu mwakilishi wake maalumu nchini Sudan Kusini na naibu mkuu wa tume ya Umoja wa Mataifa nchini humo UNIMISS. Katibu mkuu ametoa taarifa ikisema, Bw. Cong atarithi nafasi ya Bw. Moustapha Soumare kutoka Mali ambaye katibu mkuu amemshukuru kwa kazi nzuri aliyofanya nchini Sudan Kusini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |