Waziri wa fedha wa Uganda Bw. Matia Kasaija amesema, nchi hiyo inafanya mazungumzo na Kenya kuhusu kupungua kwa utoaji wa mafuta. Bw. Kasaija ameliambia bunge kuwa akiba ya mafuta ya Uganda inaendelea kupungua kutokana na kupungua kwa manunuzi ya mafuta kutoka bandari ya Mombasa ya Kenya. Amesema, wamewasiliana na serikali ya Kenya na wanafanya kila liwezekanalo kuhakikisha utoaji wa petroli na dizeli.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |