Rais Xi Jinping wa China atahudhuria mkutano maalum wa viongozi wa kundi la G20 kuhusu maambukizi ya virusi vya corona utakaofanyika kesho Alhamisi hapa Beijing.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Hua Chunying amesema mkutano huo utakaofanyika kwa njia ya video utaandaliwa na Saudi Arabia, ambayo ni nchi mwenyekiti wa zamu wa kundi hilo kwa mwaka 2020.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |