Wachezaji wa timu za Bayern Munich ya Ujerumani na wakurugenzi wao wamekubali kwa kauli moja kukatwa kwa muda asilimia 20 ya sehemu ya mishahara yao k usaidia mapambano dhidi ya virusi vya Corona. Vigogo hao wa soka Ujerumani wamesema kuwa wamefikia hatua hiyo ili kusaidia wafanyakazi wengine wa klabu hizo kifedha wakati wa kipindi hiki kigumu cha maambukizi ya virusi vya Corona vilivyosababisha kusimamishwa kwa Bundesliga na ligi zote za Ulaya. Wachezaji wa Borussia Dortmund nao wako katika mazungumzo ili kukatwa mishahara yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |