Kufuatia janga la maambukizi ya virusi vya Corona ,wachuuzi na wanaofanya biashara ndogondogo katika mitaa ya Nyeri,eneo la kati la Kenya,wamefurushwa ili kupunguza msongamano wa watu.
Wachuuzi wote na wafanyabiashara ndogondogo walifurushwa jana kutoka mtaa wa Gakere na kuamrishwa kufunga biashara zao hadi muda usiojulikana.
Mtaa huo umeonekana kuwa eneo hatari huku taifa likipambana kudhibiti usambazaji wa virusi vya Corona.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |