Rais Xi Jinping wa China amesema China inaunga mkono Shirika la Afya Duniani WHO kuonesha uongozi wake, kutunga hatua sahihi za kukinga na kudhibiti virusi vya Corona kwa njia ya kisayansi, na kuzuia kuenea kwa virusi kati ya nchi. Amesema kundi la G20 linapaswa kubadilishana taarifa zaidi kuhusu habari za kupambana na maambukizi ya virusi hivyo, kutoa miongozo ya hatua zenye ufanisi na za pande zote, na kuandaa mikutano ya ngazi ya juu kuhusu usalama wa afya ya umma duniani katika wakati mwafaka. Amesisitiza kuwa China itashirikiana na kuziunga mkono nchi husika na mashirika ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |